Untitled Document
home | tume | utangazaaji | znz

Lionel Messi avunja rekodi nyingine

Lionel Messi alikua mchezaji wa kwanza kufunga katika misimu 15 ya Ligi ya mabingwa mfululizo wakati Barcelona ilidai ushindi mwembamba huko Slavia Prague.

Nahodha Messi aliipa Barca ushindi wa mapema baada ya kupata pasi kutoka kwa kiungo Arthur.

Barcelona ambao wako juu kwenye ligi ya La Liga, kwa sasa wameshinda mechi sita mfululizo kwenye michuano yote.

Matokeo hayo yanafanya kikosi cha Ernesto Valverde kuwa kinara kwenye kundi F ikiwa na alama saba kutoka kwenye michezo mitatu, alama tatu juu ya Inter Milan na Borussia Dortmund.

Timu hizo mbili zilikutana kwenye uwanja wa Giuseppe Meazza , huku Inter ikishinda 2-0. Penalti ya Martinez ikiokolewa, huku kiungo Antonio Candreve akifunga goli la ushindi.

Matokeo yake yanawaweka vijana wa Ernesto Valverde juu ya Kundi F kwa alama saba kutoka michezo mitatu, alama tatu juu ya Inter Milan na Borussia Dortmund.

Pande hizo mbili zilikutana huko San Siro kwenye mchezo mwingine wa kundi hilo, huku Inter ikishinda 2-0.

Barca walikuwa na bahati ya kupanda kileleni huku Slavia wakiwa na haki ya kutoka na ushindi.
BBC SWAHILI.

Habari zaidi za Michezo